KILIMO CHA MATIKITI MAJI toleo la pili


UTANGULIZI

Matikiti maji ni tunda kubwa la mviringo ambalo linastawi vizuri katika maeneo ambayo ardhi yake aitwamishi maji kwa mda mrefu. Matikiti maji ni mojawapo ya jamii aina ya matunda au mbogaboga inayotambaa. Mimea hii inapatikana katika kundi linalojumuisha mimea mingine kama kama matango,maboga na maskwash. Zao la tikitiki maji ni mojawapo ya zao ambalo lina faida kubwa sana ukilinganisha na mazao mengine kwa muda mfupi.Kuna aina mbili za matikiti maji moja tikikiti lenye mbegu na lisilo na mbegu.

Tikiti maji linahitaji vitu vitano muhimu ili uweze kuzalisha kwa wingi kama

1.mwanga wa jua wa kutosha kwa maana hiyo eneo linatakiwa lisiwe na kivuli

2.Uwepo wa nyuki kwa ajiri ya uchavishaji

3.Maji ya kutosha

4.Virutubisho

5.Nafasi ya kutosha hususani katika upandaji

 

Mahitaji muhimu

1.Hali ya hewa

Matikiti maji yanahitaji kipindi kirefu cha hali ya ujoto.Kukiwa na hali ya ubaridi na mvua nyingi ina madhara kwa tikitikimaji ambayo inasababisha ukuaji hafifu,kuchelewa kukomaaa,ukuaji mbovu wa tunda na pia husababisha tunda kuwa na uwazi katikati.

2.Hali ya udongo

Tikiti maji linahitaji udongo ambao hautuamish maji kwa kipindi kirefu aina ya udongo huo ni kichanga au kichanga tifitifu…Shamba likiwa na udongo ambao unatuamisha maji kwa mda mrefu(mfinyazi sana) husababisha ukuaji wa taratibu wa zao na pia husababisha kupasuka kwa tunda.Hali ya uchachu kwa udongo ni pH  6 hadi 7.

3.Mbegu

Kiasi cha mbegu ni gram 500 kwa kila eka

 

Uchaguaji wa mbegu

Kitu muhimu katika mkulima ni uchaguaji wa mbegu bora,Upandaji wa mbegu ambayo haina soko hupelekea kukosa faida pindi unapo fanya mauzo

Mbegu Bora za Matikiti 

Mbegu maarufu ya tikiti ni Sukari F1, hata hivo madukani zinapatikana nyingi bora na tofauti tofauti kama vile:

  • Y F1 – kutoka Jubaeli
  • Sukari F1 – Kutoka East Africa seeds 
  • Sugar king F1 – kutoka Africasia 
  • Juliana F1 – kutoka Kiboseed 
  • Zebra F1 – Kutoka Balton 
  • Pato F1 – Kutoka Agrichem

 


Uwaandaji wa shamba

Hakikisha kuwa shamba lako limelimwa vizuri na udongo kulainika mpaka lifikie udongo wote hauna mabonge mabonge.

Upandaji wa tikiti maji

Panda mbegu 2  moja kwa moja katika kila shimo. Usipande katika kitalu kwasababu miche ya mitikiti huwa ni dhaifu sana wakati wa upandikizwaji iwapo itapandwa kwenye kitalu hivyo kupelekea kufa kwa miche hiyo. Panda umbali wa sentimeta 2 chini ya udongo kwa umbali wa mita 1 hadi 2 kutoka shina hadi shina na mita 1.5 – 3 kutoka mstari hadi mstari.


Zingatia: usitumie mbegu za tikiti ulilonunua (kwa ajili ya kula) kwasababu linaweza kuwa ni chotara (Hybrid) ambayo hupelekea kushusha kiasi na ubora wa matikiti yatakayo zaliwa kwa sababu yatakuwa ni kizazi cha pili (F2).

 

Katika kilimo cha umwagiliaji

1.umwagiliaji wa kutumia mifereji

2.Umwagiliaji wa kutumia matone


 

Kuweka mbolea

1.kupandia

Weka samadi kiasi cha ton 8 kwa eka kabla mlimo wa mwisho…ili kuwezesha udongo na samadi vichanganyikane.

Tumia mbolea ya dukani mfano NPK,DAP na MOP   katika mda wa kupanda mbegu.

 

2.Kukuzia

 Tumia mbolea za kukuzia ili kupata mavuno mengi

 

Zingatia

·         Ucheleweshaji au uwekaji kiasi kikubwa cha  mbolea za nitrojen husababisha kuwa na uwazi katikati wa tikitiki hii utokea kwenye kipindi cha baridi

·         uwekaji kiasi kikubwa cha  mbolea za nitrojen husababisha idadi kubwa ya mauwa dume hupelekea matunda machache

·       

 

KWA HILO TUNA MSHAULI MKULIMA KUPIMA UDONGO WAKE KWANZA ILI AWEZE KUWEKA KIWANGO SAHIHI CHA VIRUTUBISHO

 

Shughuli nyenginezo

1.Utoaji wa magugu

2.Kupruni(pitching)

3.Uchavishaji

4.Mavuno

 

Wadudu na magonjwa
Kwa kawaida zao hili halina wadudu na magonjwa mengi yanayolishambulia. Hii hutegemeana na uchaguzi sahihi wa eneo linalofaa kwa kilimo cha zao hili pamoja na hali ya hewa. Pamoja na hayo kuna baadhi ya wadudu ambao wamezoeleka katika zao hili.
Wadudu wa matikiti wako wa aina mbalimbali na wanaoshambulia sehemu wanaoshambulia majani na maua, na wengine hushambulia matunda , pia kuna magonjwa ya fangasi ambayo hushambulia mimea. Magonjwa kama Ukungu wa unga (powdery mildew) na wa chini (Downy mildew) na mengine yathibitiwe kabla hayajaleta madhara kwenye mimea.Ili kujua dawa za magonjwa ni vizuri kuchukua sampuli na kwenda nayo kwenye duka la dawa na pembejeo za kilimo ili kupata dawa sahihi. Dawa aina ya Mancozeb inaweza kutumiwa kuthibiti ugonjwa magonjwa hayo hapo juu.
Vilevile matikiti hushambuliwa na wadudu ambao hukaa katika majani, maua na matunda.
Dawa aina ya abernil,ninja,dudu all,actara,farmerguld itasaidia kuua wadudu wa majani, maua na matunda.
Vidukari: Wadudu hawa ni moja ya wadudu waliozoeleka kwenye matikiti, hushambulia sana zao hili na mara nyingi wasipodhibitiwa mapema Kabla ya kupanda hakikisha kuwa udongo una joto la wastani wa nyuzi joto 70°C. Unaweza kupanda kwa kutumia jembe la mkono au reki. Fukia mbegu kwenye mashimo kwa kutumia udongo laini na shimo lisiwe na kina kirefu, liwe na wastani wa inchi 1, ili kutoa urahisi kwa mbegu kuota.
Kwa kawaida tikiti hupandwa kwa mstari mmoja kwenye tuta lenye mwinuko wa inchi 6 na upana wa futi 4. Nafasi kati ya mche na mche iwe ni sentimita 120.

 

Ugonjwa
Zao hili hushambuliwa zaidi na ugonjwa wa Ubwiri unga. Ugonjwa huu ni hatari sana na usipodhibitiwa mapema kwa kuwa hushambulia majani ya mmea, husababisha mmea kufa baada ya muda mfupi jambo ambalo huathiri mavuno.Ni vigumu sana kuzalisha zao hili wakati wa msimu wa mvua, hivyo inashauriwa kupanda wakati wa kiangazi. Hali hii itasaidia mazao haya kustawi vizuri, ikiwa ni pamoja na kuepuka matunda kuoza kutokana na mvua kuwa matunda ya tikiti hukaa chini kwenye udongo.

 

Wadudu

Inzi wa matikiti
hawa wadudu ni waharibifu kweli kweli na uharibifu wake hufanywa usiku.Uwaribifu huanza kipindi matikiti yanapoanza kutoa mauwa na ndo kipindi muhimu tikiti kuanza kutoa vitoto.Nzi jike hutaga mayai katika tikiti dogo na kusababisha muozo ndani ya hilo tunda.

Jinsi ya kugundua kama umevamiwa na hao inzi
1.utaona doa/doti nyeusi mbili kwenye kitoto 



2.Utaona muozo na pia kudondoka kwa tikiti hilo

3.Husababosha tunda kuwa na umbo baya



JINSI YA KUZUIA
Kuna njia nyingi tu ambazo zinafanya kazi vizuri sana katika kuwaondoa hawa..Katika kitabu changu cha KILIMO CHA TIKITIMAJI kimeeleza njia zinazo fanya kazi kwa aslimia 100 ya  jinsi ya kuwandoa hawa wadudu shambani kwako..Hicho kitabu kinapatikana kwa mfumo wa EBOOK tunakutumia kwa njia ya whatsapp..Jinsi ya kukipata tuma message au piga simu kwa namba 0769550328. 




Uvunaji Matikiti
Kabla ya kuvuna matunda ni vema kwanza kujua kuwa matikiti huchukua takribani miezi mitatu mpaka mitano toka inapopandwa mpaka kukomaa. Hii hutegemea na aina ya matikiti yenyewe. Tikiti lililo komaa linaatakiwa na mwonekano wake huwa kama ifuatavyo;
Rangi ya mng’ao hupotea Upande wa chini wa tunda huanza kuwa na rangi ya njano.Pia kikonyo juu ya tunda hukauka kabisa na kuwa kijivu. Ila njia nzuri ni kuyapiga kwa kiganja na kusikiliza mlio wake unakuwa kama mlio wa ngoma.Tumia kisu wakati wa kuvuna matikiti, yabebwe na kuhifadhiwa vizuri kwenye makasha tayari kuuzwa au kwa matumizi binafsi

 

 

Sio ugonjwa lakini ni tabia yaki phisiolojia

1.Shingo ya chupa

2.Kunyauka kwa kitako

3.Kupasuka kwa tunda

4.Michirizi ya rangi nyeupe


UKITAKA MAELEZO ZAIDI TUNA KITABU CHA KILIMO CHA TIKITIMAJI  AMBACHO KINAPATIKANA KWA BEI YA PUNGUZO..WASILIANA NASI KWA NAMBA HIZO HAPO CHINI


kwa nini nakushauri uwe na kitabu hichi
1.utajifunza kuandaa shamba kitaalamu
2.utajifunza mbegu nzuri ya tikitimaji ambayo ipo sokoni kwa sasa
3.kama ujawahi lima utaona mchanganuo wa bajeti katika ekari 1
4.kama ujawahi lima utaweza kujua ratiba ya shambani ambayo inaeleza shughuli na siku sahihi
5.utajua jinsi ya kuzibiti wadudu na magonjwa yanayosumbua katika zao la tikiti
6.Utajua mbinu za kuongeza mavuno ambazo hufichwa sana

Utapokinunua hiki kitabu utapewa ushauri toka mwanzo hadi mwisho bure kabisa,ko kwa maana hiyo nina hitaji watu kumi tu..Baada ya kufika hao watu sitakiuza mpaka mda mwengne.
Hicho kitabu kinapatikana kwa mfumo wa EBOOK tunakutumia kwa njia ya whatsapp..Jinsi ya kukipata tuma message au piga simu kwa namba 0769550328. 



HUDUMA AMBAZO TUNAZITOA

1.Ushauri wa kitaalamu kuhusu kilimo Cha matikiti kutoka uchaguaji wa mbegu hadi kuvuna.

2.Ushauri jinsi ya kupambana na visumbufu shambani mfano wadudu,panya,magonjwa.

3.Ushauri wa gharama za ulimaji wa zao la tikiti kwa wale ambao hawajai kulima

4.Kumtembelea mkulima shambani ili kutoa ushauri kwa jinsi shamba linavyoonekana

5.Kutoa msaada kwa upatikanaji wa pembejeo Kama mbolea,sumu ya wadud na ukungu.

6.Huuzaji wa mitego ya kudhibiti inzi wa matikiti

 Lengo kubwa ni kulima kilimo chenye tija ambacho kinaambatana utoaji wa tikiti kubwa na Bora



MAWASILIANO

kwa whatsapp au njia ya kawaida

Mtaalamu OBEDI KAYANGE   

PIGA  0769550328

Whatsapp 0769550328

           

Mtaalamu AMANI KINGU   

0766298379

Barua pepe  

cheteagrosolution@gmail.com

KARIBU SANA 


kilimo ni chetu sote



Comments

  1. Hongera sana kwa maelezo mazuri, karibu shambani utushauri zaidi tuweze kupata mazao mengi zaidi ili tujenge uchumi wetu na wa nchi kwa ujumla

    ReplyDelete
  2. Nakubl boss wangu mr.fusalium kaz nzur bravoo broo

    ReplyDelete
  3. Nimeupenda Sana taaluma yako uko vzr sana

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

Kilimo Bora Cha Matikiti Maji

JIFUNZE KUHUSU KILIMO CHA KISASA CHA MATUNDA