JIFUNZE KUHUSU KILIMO CHA KISASA CHA MATUNDA






KILIMO CHA MATUNDA

Kilimo ambacho kinakua kwa kasi sana kwa Tanzania na kwa Dunia kiujumla,Uhuhitaji wa matunda kwa matumizi ya nyumbani na kiwandani huongezeka mara dufu kadri siku zinavyoenda.Hichi kilimo kinahusisha miti ambayo huchukua miaka miwili hadi mitatu mpaka kufikia mavuno.

Kilimo cha matunda kinaumuhimu mkubwa sana kama

                                i.   Kuongeza kipato endelevu kwa mkulima

                              ii.kuongeza uhakika wa chakula

                            iii.kupungua hewa ya ukaa,

                             iv.kupunguza ongezeko la joto, na kuboresha mkusanyiko wa mawingu ya mvua,

                               v.  kuimarisha utunzaji wa maji aridhini katika maeneo ya mashambani

                             vi.   Hakina gharama kubwa katika utunzaji

Hivyo basi elimu ya utunzaji mzuri wa bustani za matunda ni muhimu ili kuweka mazingira mazuri ya uoto wa kijani, kuhifadhi ardhi na kujihami na mabadiliko ya tabia nchi.

SIFA ZA MATUNDA

§  Ukubwa wa tunda/ Uzito wa tunda

§  Utamu wa tunda

§  Kiwango cha mafuta (parachichi)

§  Udogo wa mbegu (Embe na parachichi)

§  Rangi ya ganda la tunda likiwa bichi au linapoiva (embe na parachichi)

§  Urahisi wa kumenya ganda (parachichi)

§  Ugumu wa ganda kuvumilia kubonyezwa (parachichi, chungwa)

§  Unene wa ganda (parachichi, chungwa)

§  Kuwa au kutokuwa na mbegu (chungwa)

 

SIFA ZA MITI YA MITUNDA

§  Kuzaa mapema

§  Matunda kuwahi kuiva/kukomaa ndani ya msimu

§  Mti kuwa mkubwa

§  Mti kuzaa mara mbili au zaidi kwa mwaka

§  Kuvumilia ukame

§  Kuhifadhi matunda kwa muda mrefu baada ya kukomaa/kuiva bila kudondoka

Zifa hizi na nyinginezo huwa na maana kwa jamii hasa kwa sababu za kibiashara na matumizzi. Kwa mfano,miembe dodo ambayo huwa na matunda makubwa huuzwa kwa bei ya juu, hivyohutumika kama zao la biashara zaidi kuliko kuliwa nyumbani/shambani, kama ilivyo kwa embe aina ndogo ndogo kama sindano. Aina ndogo za embe zinapoiva hata watoto wanazipata kwa urahisi na kula. Kwa upande mwingine, embe ndogo kama sindano, huzaa matunda mengi, hata wakati wa hali mbaya a hewa.

 

AINA YA MICHE YA MATUNDA

1.      Miembe

§  Tomyy

§  Red India

§  Apple Mango

§  Dodo

§  Bolibo

§  Alphonso

§  kenti

2.Ndizi

 

3.Parachichi

4.Topetope

5.Fenesi

6.Pesheni

7.Komamanga

8. Mbilimbi

9.  Chenza

10.Ndimu

 

 

11.Papai

§  Malkia  F1

§  Calphonia

12.  Tende

13.  Sherisheri

14.  Zaituni

15.Michungwa

 

16.Limao

17.Tini

18.peasi

 

19.Pera

 






UCHIMBAJI WA MASHIMO NA KUPANDA

Shimo linashauriwa liwe refu wastani kwa 0.6mX0.6mX0.6m(UPANA 0.6mX0.6m,UREFU 0.6m), hata chini ya hapo kulingana na hali ya udongo (rutuba, aina ya udongo nk).

Wakati wa uchimbaji wa mashimo haya, udongo wenye rutuba  (wa juu) ni lazima utenganishwe na udongo wa chini. Weka udongo wa juu sehemu ya mwinuko na wa chini sehemu ya mteremko ili kukumbuka. Mashimo haya huandaliwa/huchimbwa halafu hujazwa debe moja/ndoo ya lita 20 za mboji hususani maeneo yaliyo na rutuba dhaifu. Unaweza kuweka debe moja hadi tatu za samadi au mboji iliyoiva kikamilifu kutokana na aina na rutuba ya udongo.

Mbolea ambayo haijaoza vizuri ni hatari kwani yaweza kuunguza mizizi ya miche.Mara nyingine hulazimu kuandaa shamba na kupanda siku zijazo. Kama hili litatokea, mkulima anashauriwa kuweka mambo (kijiti) katikati ya shimo kama alama ya katikati ya shimo hivyo kurahisisha upandaji wakati ufikapo.



BAADHI YA MICHE NA IDADI KWA KILA EKARI

Kwa kuzingatia nafasi za kila mche katika ekari unapata idadi ya miche

AINA MCHE

IDADI YA MCHE

Embe

miche 64

Parachichi

miche 64

Chungwa

miche 200

Cheza

miche 200

Ndimu

miche 200

limao

miche 200

topetope

miche 200

fenesi

miche 200



UPANDAJI WA MICHE

Wakati wa kupanda, ni lazima kukata mizizi yote iliyotokeza nje ya kiriba kabla ya kutoa mche. Hii husaidia ukuaji wa mizizi mipya na kurahisisha utoaji wa mche kwenye mfuko. Toa mche taratibu na hakikisha kikulia mmea hakitengani na mizizi. Miche hupandwa kwa usawa wa kina kilekile kama ilivyokuwa kitaluni.

 Epuka kupanda miche chini zaidi ya ilivyokuwa kwenye kiroba kwani yaweza kusababisha kushambuliwa na magojwa na kufa. Sehemu iliyobebeshwa ni lazima iwe juu ya ardhi kwa kiasi kisiasi cha 10-20 sm. Sehemu hii haitakiwi ifike kwenye udongo. Ikitokea hivyo, kitawi kilichobeshwa kinaweza kutoa mizizi yake na kisha kuharibu maunganisho. Pia sehemu hii ni rahisi kushambuliwa na wadudu wasababishao magonjwa Shimo hufukiwa hadi kufikia sehemu uliyotenganisha mizizi na shina kwa kushindilia udongo.


Upandaji unashauriwa kufanyika mwanzoni mwa mvua ndefu za masika ili miche iweze kupata maji ya kutosha kabla kiangazi kuanza. Tengeneza Kuzunguka miche iliyopandwa visahani na kuvifunika na majani makavu ili kurahisisha umwagiliaji ikiwa ni kipindi cha kiangazi, kuzuia unyevu usipotee na kupunguza joto ardhini. Weka miti ya kuizuia miche isianguke hasa kama miche inagusa ardhi. Kwa ujumla, inashauriwa kuwa na kinga dhidi ya upepo/kimbunga. Hii inasaidia kuepusha kuvunjika kwa miche michanga na hata miti mikubwa hususan wakati inapokuwa imezaa. Kwa maeneo yenye upepo mkali, ni vizuri kuotesha miti ya kuzuia upepo mapema mwaka 1-2 kabla ya kuotesha miche yako. Ni muhimu sana kumwagilia kikamilifu miche yako punde baada ya kuipanda shambani hata kama dalili zinaonesha kuna uwezekano wa mvua kunyesha.



BAADA YA KUPANDA

Umwagiliaji.
Utunzaji wa miche baada ya kupanda ni kama ulivyo kwa miti mingine ya matunda. Umwagiliaji wakati wa kiangazi ni muhimu sana. Maji kiasi cha lita 15-20 kwa kila mche kwa wiki huchukuliwa kama kiwango kizuri ila inategemeana na hali ya hewa na aina ya udongo(utaruhusiwa kumwagilia kwa mara nyingine pindi unyevu wa udongo unapopotea). Kuweka maji mengi sana kwenye visahani vya miche yaweza kusababisha madhara sawa au zaidi ya yale ya kuweka maji yasiyotosheleza. Kila mara angalia unyevu uliopo kabla ya kuweka maji shambani na epuka kuweka maji kiasi kwamba yanatuama kwenye visahani.


Kuwekea matandazo

Ni vizuri kutandaza majani makavu kuzunguka miche. Hii ni muhimu kuhifadhi unyevu na kuzuia magugu kuota. Matandazo haya ni muhimu yasigusane na miche ili kupunguza athari za mchwa pamoja na kuepusha unyevu wa muda mrefu kwenye shina ambao huweza kuleta magonjwa.




HUDUMA AMBAZO TUNATOA

                             i.            UUZAJI WA MICHE YA MATUNDA YA MDA MFUPI

                           ii.            MAELEKEZO YA JINSI KUANZISHA SHAMBA KWA AJILI YA KILIMO CHA MATUNDA

                         iii.            KUTEMBELEA MASHAMBA YA MATUNDA KWA KUTOA USHAURI NA HUDUMA NYENGINEZO



 

TUNAPATIKANA KARIBU NA CHUO KIKUU CHA KILIMO SOKOINE (SUA) MOROGORO,BARABARA YA BOMA(BOMA ROAD)…KWA MAHITAJI YA MICHE POPOTE TUNATUMA NDANI YA TANZANIA

MAWASILIANO

PIGA  0769550328

Whatsapp 0769550328














Comments

  1. mnavyo vitabu vinavyoelekeza kufanya grafting?

    ReplyDelete
  2. Nikihitaji kitabu naweza kukipata au hajaviandaa nipo dodoma

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

Kilimo Bora Cha Matikiti Maji

KILIMO CHA MATIKITI MAJI toleo la pili