Embe ni zao lenye fursa kubwa sana ya kumwinua mjasiriamali





Kwa ufupi
Kampuni ya matunda ya Natureripe ya Kilimanjaro yenye makao yake makuu jijini Dar es Salaam inasema embe ni zao ambalo lina fursa za kumuinua mtu kiuchumi tena kwa haraka bila kutumia nguvu.

Ni ajabu kuona kuwa Watanzania wengi wamekuwa hawaweki kipaumbele kwenye kilimo cha embe. Wengi wanapenda kilimo cha kahawa, pamba, korosho, lakini embe hapana.
Hali hiyo imetokana na kilimo kukosa tija, na kutokuwapo kwa soko la uhakika la maembe.
Kutokana na hali hiyo maembe mengi yanaozea mashambani kwa kukosa soko la uhakika na kusababisha wengi kutokutoa kipaumbele katika zao hilo.
Kampuni ya matunda ya Natureripe ya Kilimanjaro yenye makao yake makuu jijini Dar es Salaam inasema embe ni zao ambalo lina fursa za kumuinua mtu kiuchumi tena kwa haraka bila kutumia nguvu.

Embe lina soko kubwa
Mkurugenzi wa Natureripe, Fatma Riyami anasema embe ni zao lenye soko kubwa duniani na linaweza kumwingizia mtu fedha nyingi kwa kipindi kifupi.
“Tofauti na mazao mengine, unawekeza fedha kidogo kwenye uzalishaji wa embe, lakini unapata fedha nyingi kwa mkupuo,” anasema Riyami.
Riyami anasema siyo aina zote za embe zina soko bali zenye soko kubwa duniani ni zile  ambazo hazina nyuzinyuzi.
Embe nyingi zinazozalishwa nchini zina nyuzinyuzi nyingi ambazo hazina wanunuzi kwenye soko la kimataifa kwa sababu zinakwama kwenye meno na kusababisha shida ya kuzitoa.
Anasema mbegu ambazo hazina nyuzinyuzi tayari zimeingizwa nchini na kampuni yake na wanaziuza kwa mkulima yeyote anayezihitaji.
“Uzuri wa embe hizi ni kwamba zina zaa baada ya  miaka mitatu tangu zilipopandwa na huzaa kwa wingi kama zinatunzwa vizuri,” anasema.
Anasema mti mmoja wa embe una uwezo wa kuzaa kiwango cha embe zisizopungua 300 kwa msimu mmoja.
Kwa kawaida mbegu hizo zisizo na nyuzi zipo za aina tano ambazo ni Apple, Kent, Keitt, Palmel, na Tomy Atkinsi.
Mbegu hiyo inapandwa umbali wa mita nane na kwamba kwenye ekari moja inapandwa miche 64.
Katika shamba la maembe, yanaweza yakachanganywa mazao mengine ya muda mfupi kama vile mananasi, mipapai, matikiti maji, na jamii za mbogamboga.
Anasema kadri mwembe unavyokuwa, matawi yanapaswa kupunguzwa ili yasirefuke na mkulima avune matunda ya mti huo bila kupanda mtini.
Kuhusu mbolea anasema inategemea ushauri wa kitaalamu kulingana na aina ya udongo wa shamba linalotumika.
Pia dawa ni muhimu kwa ajili ya kuua wadudu wanaosababisha maua kupukutika au matunda kuoza.
Anasema wakulima watakaofika kununua mbegu hizo watapewa elimu ya kilimo hicho, ushauri na namna ya kupata masoko wakati wa mavuno.
Kampuni ya Natureripe licha ya kulima embe pia inanunua embe za wakulima na kuuza katika masoko ya kimataifa hasa nchi za Mashariki ya Kati.
Aina za miti ya maembe
Zipo aina nyingi za embe,  hapa,  tumeelezea chache tu,  ambazo ni nzuri kibiashara. 
apple: Aina hii ya maembe asili yake ni pwani ya Kenya. Ina rangi nzuri ya njano au rangi ya chungwa inapoiva, matunda haya ni ya kiwango cha kati na kubwa, yenye muonekano wa mviringo na ngozi laini, na hayana nyuzi kabisa. Aina hii ina soko zuri, na inazaa sana
Kent: Aina hii ina rangi ya kijani na njano nzuri inayovutia kwenye sehemu ya juu. Maembe haya ni rojo rojo na nyama yake ni ya njano iliyokolea na hayana nyuzi nyuzi, yana ladha nzuri sana. Miti yake ina umbo kubwa iliyo nyooka kwenda juu na ni mazuri kwa kuuza nje ya nchi. 
Tommy Atkins: Aina hii imekuwa maarufu sana kibiashara. Maembe haya ni magumu kiasi, yana njano iliyokolea, maji maji ya kiasi, na nyuzi za kiasi, pamoja na harufu nzuri. Ni aina nzuri kwa kuuza nje ya nchi kwa kuwa inastahimili kukaa muda mrefu bila kuharibika. Aina hii pia inaweza kukabiliana na ugonjwa wa kimamba na madoa madoa ya kubambuka. 
Keitt: Aina hii ina ubora wa pekee katika kuhifadhiwa na inaweza kuachwa juu ya mti kwa muda mrefu hata baada ya muda wa kawaida wa msimu kupita. Matunda yake ni makubwa, na yanakuwa na rangi ya kijani na njano, au nyekundu iliyofifia. Ina kiasi kikubwa cha weupe, au njano/ nyekundu kwenye ganda lake ambalo ni nene na gumu. Tunda lake lina umbo kama yai na lenye mviringo mzuri, na halina mdomo mgumu, kikalio chake ni cha mviringo. Mti wake una umbo la kati na huwa na matawi marefu yanayojikunja, na yana nafasi inayoruhusu kuonekana vizuri, na yana uwezo wa kubeba uzito mkubwa. Aina hii ina soko zuri, na inazaa sana na pia ina uwezo wa kukabiliana na ugonjwa wa madoa doa ya kubambuka.

Faida ya kulima embe
Katika msimu uliopita walinunua embe moja kutoka kwa wakulima kwa Sh100.
“Ina maana kwamba kwa mkulima mwenye shamba la ekari moja lenye miche 64 ambalo limezaa maembe 300 kwa mti mmoja. Mkulima atapata Sh1.9 milioni,” anasema Riyami.
Anasema ekari moja inagharimu Sh300,000 kupanda mpaka kuvuna na mkulima kupata faida ya Sh Sh1.6 milioni.
Kampuni hiyo pia inasindika matunda ya embe ili kutengeneza bidhaa mbalimbali.
“Hivi sasa tunatengeneza chachandu inayotokana na embe. Tunazo aina tatu zinazojulikana kama Mango Pilipili, Mango Zodo na Mango Pickle,” anasema Riyami.
Pia wana mpango wa kusindika embe kwa ajili ya kutengeneza juisi  ambazo hazina kemikali.
Wakati wa maonyesho ya kuonja embe yaliyofanyika jijini Dar es Salaam mwanzoni mwa mwaka huu, Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima wa Embe nchini(Amagro) Burton Nsape anasema kuwa chama hicho kinawasaidia wakulima wa embe kujipatia kipato kupitia zao hilo na pia hutoa elimu kwa wanachama wake kuhusiana na kilimo cha embe.
Nsape anasema changamoto kubwa inayowakabili wakulima wa embe nchini ni ukosefu wa kusafirisha kitaalamu kutoka mashambani hadi sokoni.

Karibu ujipatie Miche bora ya miembe ya kisasa, aina hizo hapo juu na nyingne. 
Pia tunayo miche ya matunda mengine kama Papai, parachichi, Michungwa, Migomba. Miche yote hii ni ya kisasa na ni ya muda mfupi.
Pamoja na Miche utapatiwa ushauri wa kitaalamu. 
Vitalu vyetu vya miche vinapatikana  Morogoro. Kwa wateja wa mikoani tunatuma, na miche inafika salama kabisa




Mawasiliano: Simu 0769255000



Comments

  1. Tazari tunaomba namba za mawasiliano yenu pamoja na anwani

    ReplyDelete
  2. Maelezo yako nimeyapenda, naomba uongeze bei za miche ili tujue gharama zako.

    ReplyDelete
  3. Nitawatembelea na kununua Miche

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

Kilimo Bora Cha Matikiti Maji

KILIMO CHA MATIKITI MAJI toleo la pili

JIFUNZE KUHUSU KILIMO CHA KISASA CHA MATUNDA