Posts

Showing posts from August, 2018

Kilimo Bora Cha Matikiti Maji

Image
Matikiti maji hulimwa kama zao la biashara katika sehemu nyingi duniani zenye hali ya hewa ya joto la wastani. Zao hili lina wapatia watu shughuri za kufanya na hivyo kuwapatia kipato kuanzia kwenye nyanja za uzalishaji hadi kwenye matumizi. Matikiti maji ni mojawapo ya jamii aina ya matunda au mbogaboga inayotambaa. Mbegu Bora za Matikiti  Mbegu maarufu ya tikiti ni  Sukari F1 , hata hivo madukani zinapatikana nyingi bora na tofauti tofauti kama vile: Arashani F1  – kutoka Syngenta  Sukari F1  – Kutoka East Africa seeds  Sugar king F1  – kutoka Africasia  Juliana F1  – kutoka Kiboseed  Zebra F1  – Kutoka Balton  Pato F1  – Kutoka Agrichem MAHITAJI YA TIKITIMAJI Tikiti linakua vizuri katika udongo unaoshika maji vizuri lakini yasio tuama na kuruhusu mzunguko mzuri wa hewa na maji.Udongo wenye pH 5.8-6.6.pia kama pH ni ndogo tutakushauri cha kufanya ili iweze kuwa nzuri na ya kiasi kwa ajili tikitimaji.  Tikiti halistawi vyema ktk baridi na linahitaji joto la udongo

KILIMO CHA BUSTANI AMBACHO HAKIHITAJI ENEO KUBWA

Image
Habari ndugu msomaji wa wetu wa makala za kilimo, Natumaini tunaendelea vizuri na mapambano ya kila siku. Leo tutaanza kujifunza kilimo cha bora cha mboga mboga ambacho :  hakiitaji eneo kubwa  huzalisha mboga kwa wingi   hautaji kuwa na maji mengi ya umwagiliaji Inapunguza utumiaji wa kemikali za viwandani Gharama za uhitaji wa mboga za majani. inatumia nafasi ndogo na kutoa kiasi kikubwa cha  mboga mboga. na tutaanza kufahamu vitu vya msingi kwanza, na natumaini ukimaliza mfululizo wa makala hizi utakua mkulima hodari wa nyanya. Kila kitu lazima kiwe na msingi imara, karibu tujifunze wote: Vifaa: Udongo, Kokoto (mawe madogo madogo), Gunia, mchanga/Pumba za mpunga (Rice husk), Mbole ya samadi iliooza vizuri, mti/mbao na kopo dogo (sadolini). Udongo - Kwa ajili ya kuwezesha mmea kusimama, pia kupatia virutubisho mmea Mchanga/Rice husk - Kusaidia mizizi kupita kwa urahisi, pia kuweka mazingira mazuri ya hewa na maji katika udongo yaani mzunguko wa maji na hewa.

PANDA MICHE YA MATUNDA,YENYE TIJA

Image
NI MICHE AMBAYO IMEFANYIWA GRAFTING YENYE UWEZO WA KUTOA MATUNDA MENGI KWA MDA MFUPI NA   KATIKA VITALU VYETU TUNA MICHE ZAIDI YA KUMI NA MOJA AMBAYO NI : 1.EMBE 2.MGOMBA 3.PAPAI ZA MDA MFUPI 4.CHENZA 5.LIMAO 6.CHUNGWA 7.PARACHICHI 8.PERA 9.FENESI 10.TOPETOPE 12,MZAITUNI Kama unahitaji miche ya matunda sasa unaeza kuwasiliana nami hata  uliopo mkoani mzigo unafika ...Tupo Morogoro-MAENEO YA SUA. 0769550328 kwa kujifunza kilimo chenye tija,utakutana wataalamu na wakulima bonya hapa chini JIUNGE NA GROUP LA WHATSAPP

Kilimo Bora cha Nyanya

Image
Habari ndugu msomaji wa wetu wa makala za kilimo, Natumaini tunaendelea vizuri na mapambano ya kila siku. Leo tutaanza kujifunza kilimo cha bora cha nyanya, na tutaanza kufahamu vitu vya msingi kwanza, na natumaini ukimaliza mfululizo wa makala hizi utakua mkulima hodari wa nyanya. Kila kitu lazima kiwe na msingi imara, karibu tujifunze wote: Utangulizi: Uzalishaji mdogo unasababishwa na kupungua kwa rutuba ya ardhi, upepo, joto, ukame. Sababu nyingine ni pamoja na ukosefu wa aina za nyanya zenye mavuno mengi amabazo zinahimili mazingira ya kwetu, wadudu, magonjwa na magugu. Mazingira • Hali ya Hewa: Nyanya hustawi vizuri zaidi kwenye mazingira ya joto la wastani kuanzia nyuzi joto 18-27 sentigreti. Mvua nyingi husababisha mlipuko wa magonjwa ya ukungu kama vile Baka jani chelewa n.k.) • Udongo: Nyanya hustawi kwenye aina zote za udongo kuanzia udongo wa kichanga, mweupe wa tifutifu hadi udongo wa mfinyanzi, ili mradi uwe na mboji ya kutosha na usiosimamisha/tuamisha maji.