Posts

Showing posts from September, 2020

JIFUNZE KUHUSU KILIMO CHA KISASA CHA MATUNDA

Image
KILIMO CHA MATUNDA Kilimo ambacho kinakua kwa kasi sana kwa Tanzania na kwa Dunia kiujumla,Uhuhitaji wa matunda kwa matumizi ya nyumbani na kiwandani huongezeka mara dufu kadri siku zinavyoenda.Hichi kilimo kinahusisha miti ambayo huchukua miaka miwili hadi mitatu mpaka kufikia mavuno. Kilimo cha matunda kinaumuhimu mkubwa sana kama                                 i.     Kuongeza kipato endelevu kwa mkulima                               ii. kuongeza uhakika wa chakula                             iii. kupungua hewa ya ukaa,                              iv. kupunguza ongezeko la joto, na kuboresha mkusanyiko wa mawingu ya mvua,                                v.    kuimarisha utunzaji wa maji aridhini katika maeneo ya mashambani                              vi.     Hakina gharama kubwa katika utunzaji Hivyo basi elimu ya  utunzaji mzuri wa bustani za matunda ni muhimu ili kuweka mazingira mazuri ya uoto wa kijani, kuhifadhi ardhi na kujihami na mabadiliko ya tabia nchi .

KILIMO CHA VITUNGUU

Image
Utangulizi Kitunguu ni mojawapo la zao linalimwa kwa wingi na pia linawatumiaji wa kila siku nchini na nje ya nchi.  Linachukua nafasi ya pili baada ya nyanya. Kitunguu kinatumika katika kachumbari, kama kiungo kwenye kitoweo kama vile Samaki, nyama, mboga za mahani n.k. Majani ya vitunguu hutumika kama mboga. Vitnguu pia hutumika kuandalia supu.vitunguu vimetofautiana kwa rangi(nyekundu,njano na nyeupe),umbo(mviringo na bapa) na radha(tamu na punget).   Mahitaji muhimu kwenye kilimo cha vitunguu 1.Hali ya hewa Kitunguu hustawi vizuri kwenye mvua kiasi mm 500 had mm 700.Hali ya ujoto eneo hilo liwe na ujoto kiasi ambacho kinaweza kuwa nyuzi za joto 15 hadi 30,joto la kawaida sana.Endapo joto likazidi nyuzi joto 30 kitunguuu hukomaa kwa haraka kabla ya mda wake na pia kupelekea umbo kuwa dogo na mavuno kupungua .Endapo joto likawa chini sana inasababisha ukuaji wa taratibu na kitunguuu kuanza kutoa mauwa kabla ya wakati na pia hali ya baridi hupelekea magonjwa ya majani.