KILIMO CHA VITUNGUU





Utangulizi

Kitunguu ni mojawapo la zao linalimwa kwa wingi na pia linawatumiaji wa kila siku nchini na nje ya nchi.  Linachukua nafasi ya pili baada ya nyanya. Kitunguu kinatumika katika kachumbari, kama kiungo kwenye kitoweo kama vile Samaki, nyama, mboga za mahani n.k. Majani ya vitunguu hutumika kama mboga. Vitnguu pia hutumika kuandalia supu.vitunguu vimetofautiana kwa rangi(nyekundu,njano na nyeupe),umbo(mviringo na bapa) na radha(tamu na punget).

 

Mahitaji muhimu kwenye kilimo cha vitunguu

1.Hali ya hewa

Kitunguu hustawi vizuri kwenye mvua kiasi mm 500 had mm 700.Hali ya ujoto eneo hilo liwe na ujoto kiasi ambacho kinaweza kuwa nyuzi za joto 15 hadi 30,joto la kawaida sana.Endapo joto likazidi nyuzi joto 30 kitunguuu hukomaa kwa haraka kabla ya mda wake na pia kupelekea umbo kuwa dogo na mavuno kupungua.Endapo joto likawa chini sana inasababisha ukuaji wa taratibu na kitunguuu kuanza kutoa mauwa kabla ya wakati na pia hali ya baridi hupelekea magonjwa ya majani.

 

2.Udongo

Kitunguu kinahitaji udongo wenye rutuba ambao hautwamishi maji kwa mda mrefu ambao ni kichanga tifutifu na uchachu wa udongo unatakiwa pH 6 hadi 8.

 

Uchaguaji wa mbegu bora

Kama wataalamu wa kilimo tunashauri mkulima anunue mbegu bora kutoka kwenye kampuni yenye kuaminika.Mbegu bora inamanufaa makubwa sana kwa sababu ndo chanzo cha ongezeko la mavuno shambani kwako.

Kuna aina nyingi za mbegu za vitunguu lakini mimi katika makala yangu nitaeleza mbili tu ambazo ni RED BOMBAY na RED CREOLE

1.Red Bombay

        i.            Ni mbegu ambayo inafanya vizuri zaidi maeneo yenye hali  ya  ukavu na ujoto

      ii.            Inatoa vitunguu kuanzia size ya ndogo hadi ya kati,rangi ya zambarau nyekundu  iliyo kolea na umbo la dunia

    iii.            Inakomaa siku 150 baada ya kupandikiza kutoka kwenye kitalu

    iv.            Inatoa mavuno wastani  wa kilo 16000 kwa ekari

 

2.Red creole

        i.            Inatoa vitunguu rangi ya nyekundu  na umbo la bapa mzunguko

      ii.            Inakomaa siku 150 baada ya kupandikiza kutoka kwenye kitalu

    iii.            Inakaa mda mrefu gharani au hairabiki haraka baada ya kuvunwa

    iv.            Inatoa mavuno wastani  wa kilo 16000 kwa ekari

 

Uwandaaji wa shamba

Hakikisha kuwa shamba lako limelimwa vizuri na udongo kulainika mpaka lifikie udongo wote hauna mabonge mabonge.

 

Uwandaaji wa kitalu

Weka tuta lenye upana wa mita 1 changanya na mbolea ya samadi kilo 20 kwa mita 1 za mraba na pia weka na mbolea ya kupandia DAP/TSP gram 20 kwa mita 1 za mraba.Na pia nafasi kati ya tuta moja na jengine ni sm50 na urefu wa huo mfereji ni sm1 .Kiasi cha mbegu ni gram 800 hadi 1200 kwa ekari inapandwa kwenye kitalu bila kusahau matandazo.Mbegu hutumia siku 7  hadi 10 maotea kuonekana.

 

Katika kuhudumia kitalu mwagilia kitalu chako kwa mpangilio baada maotea kuonekana,,toa matandazo,weka kichanja kwa kila tuta ili kuzuia jua.Na pia fanya kutoa magugu,dhibiti magonjwa na wadudu pindi dalili zinapoonekana.

 

Kupandikiza

1.mda  wa kupandikiza

Mche unapandwa baada ya wiki 6 hadi 8 baada ya kupanda au ukifika majani 3 hadi 5 pindi kitako kinakuwa unene kama penseli

2.Nafasi kwa kila mche

Mche unapandwa kwenye shimo la sm 2.5 hadi 3 na pia kati ya msitari mmoja na mwengine sm30 na pia kati ya mche mmoja na mwengine sm8 hadi sm10.

3.Njia zakupandikiza

Mwagilia kabla ujatoa mche kutoka kwenye kitalu,vuta taratibu mche kutoka kwenye kitalu ili usiharibike,unapopanda mche usifukie udongo zaidi ya inchi moja.





Katika kilimo cha umwagiliaji

Kitunguu kinaitaji umwagiliaji mwepesi na wakila mara ambao upo katika utaritibu maalumu

1.katika hatua ya ukuaji -------Umwagiliaji wa maji mengi unatakiwa kuzuiliwa

2.katika hatua ya  utungaji wa kiazi-----tunahitaji kumwagilia maji mengi

3.katika kipindi cha kukomaa-----tunatakiwa kupunguza au kuacha kabisa kumwagilia

Zingatia:kumwagilia kwa mpangilio maaulumu unasaidia kuondoa tatizo la mzizi kuwa ya pinki,inaimalisha afya ya mizizi na pia ukuaji kitunguu ulio bora.

Ukosefu wa unyevu husababisha kitunguu kukatika au kuundwa kwa vitunguu viwili katika mmea mmoja.

 

Kuweka mbolea

1.kupandia

Weka samadi kiasi cha tan 10 hadi 16  na tumia jembe kwa ajili yakuchanganya na samadi inatakiwa kuwekwa wiki moja hadi mbili kabla ya kupandikiza,kitunguu kinafanya vizuri kama ukiweka samadi.

Tumia mifuko miwili ya mbolea ya DAP/TSP   au NPK kwa eka  katika mda wa kupandikiza.

 

2.Kukuzia

Hili tunashauri mkulima atumie njia ya kuweka karibu na mmea lakini usigusane kuliko njia yakutawanya.Tumegawa katika vipindi viwili

Kipindi cha kwanza---hii inafanyika siku30 baada ya kupandikizwa ambayo ni mifuko mmoja ambayo ni UREA

Kipindi cha pili----hii inafanyika siku 45 baada ya kupandikizwa ambayo ni mfuko mwili ya CAN

Zingatia: uwekaji wa kiasi kikubwa cha nitrojeni husababisha shingo nene na uwekaji wa mbolea umalizike kabla ya kutungwa kwa kiazi.

 

Fanya kupunguza udongo ili kufanya kutanuka kiazi vizuri hii inasadia kwenye rangi ya kitunguu na pia katika kipindi cha kuvuna.Na pia kama udongo wako ni mgumu fanya kuupunguza ili kufanya ukuaji mzuri wa kiazi.Hiii hufanyika katika parizi ya pili na inayofuata hii ifanyike kwa mkono na pia kuwa makini na mizizi ya kitungua kutoharibika.

 


Wadudu wanaoshambulia vitunguu

Kuna aina nyingi za wadudu wanaoweza kushambulia vitunguu.  Hawa wafuatao ni baadhi ya wadudu waliozoeleka kwenye zao la vitunguu.

 

1.Thiripi 

Wadudu hawa hukaa kwenye jani sehemu inayokutana na shina. Wadudu hawa hufyonza maji kwenye majani ya vitunguu na kusababisha majani kuwa na doti nyeupe.

Madhara: Husababisha vitunguu kudumaa hivyo kuathiri ukuaji wake jambo ambalo huathiri mavuno pia.

2.Kimamba

Wadudu hawa hufyonza maji kwenye vitunguu, na kusambaza ugonjwa wa virusi. Husababisha kudumaa kwa vitunguu. Wadudu hawa ni hatari zaidi kwa kuwa husambaza virusi vinavyoingia hadi kwenye mbegu.

3.Minyoo fundo

Aina hii ya minyoo hushambulia mizizi ya vitunguu. Hali hii husababisha kudumaa kwa vitunguu kwa kuwa hushindwa kufyonza maji na chakula kutoka ardhini.

4.Vidomozi

Hushambulia majani kwa kujipenyeza kwenye ngozi ya jani na kusababisha michoro ambayo huathiri utendaji wa majani.

5.Utitiri mwekundu

Wadudu hawa hufyonza maji kwenye majani na kusababisha vitunguu kunyauka.

6.Funza wakatao miche

 Funza hawa hutokana na wadudu wajulikanao kama Nondo, na hushambulia shina na kulikata kabisa.

 

Namna ya kukabiliana na wadudu hawa

Unaweza kukabiliana na wadudu hawa kwa kufanya kilimo cha mzunguko.  Usioteshe vitunguu sehemu moja kwa muda mrefu, au kufuatanisha mazao jamii ya vitunguu kama vile leaks.

Tumia mbegu bora zilizothibitishwa kutoka kwenye kampuni zinatambuliwa kisheria na kibiashara.  Kupanda kwa wakati unaotakiwa; vitunguu visipandwe wakati wa kiangazi. Vipandwe wakati wa majira ya baridi na kuvunwa wakati wa joto. Tumia dawa za asili za kuulia wadudu, au dawa nyinginezo zinazopendekezwa na wataalamu wa kilimo.

 

Magonjwa yanayoshambulia vitunguu

1. Purple blotch

Ugonjwa huu husababishwa na ukungu (fungus). Ugonjwa huu husababisha mabaka ya zambarau na meusi katika majani ya vitunguu.  Ugonjwa huu hutokea wakati wa unyevu unyevu mwingi.
Madhara: Ugonjwa huu hupunguza mavuno mpaka asilimia hamsini (50%).

Kudhibiti: Unaweza kuzuia kwa kutumia kiuwa kuvu chenye viambata Mancozeb na Difenoconazole.

 

 

2. Stemphylium leaf blight

 Hukausha majani kuanzia kwenye ncha hadio kwenye shina.; Ugonjwa huu hutokea wakati wa unyevu na ukungu mwingi.
Madhara: Hupunguza mavuno hadi kwa asilimia sabini na tano (75%).

Kudhibiti: Unaweza kuzuia kutumia kiuwa kuvu chenye kiambata cha copper

 

3. Magonjwa ya virusi

Ugonjwa huu husababisha vitunguu kuwa na rangi iliyochanganyika, kijani na michirizi myeupe au njano.  Vitunguu hudumaa kwa kiasi kikubwa;Ugonjwa huu husababishwa na kimamba.

Madhara: Huathiri mavuno kwa asilimia 80 mpaka asilimia 100%.

 

Kudhibiti: Unaweza kuzuia vimamba ambao ndio wanaoeneza virusi kwa kutumia dawa za kuulia wadudu

 

4. Kuoza kwa kiazi

Husababishwa na fangasi. Ugonjwa huu hutokea vitunguu vikishakomaa, huku udongo ukiwa na maji maji.  Vitunguu vikishakomaa visimwagiliwe tena.

 

Kudhibiti: Unaweza kuzuia kwa kuvuna mapema,fanya kilimo mzunguko,kausha baada ya kuvuna na ondoa kiazi kilicho onyesha dalili za kuoza.

 

Uharibifu wa vitunguu usiotokana na magonjwa

 1.kuchipua baada ya kuvunwa

Hali hii hutokea endapo vitunguu vitavunwa kabla ya muda wake.  Endapo vitunguu havitakaushwa vizuri baada ya kuvunwa. Hali hii husababisha uharibifu mpaka asilimia themanini (80%).  Sehemu ya kukaushia vitunguu iwe na hewa inayozunguka na mwanga wa kutosha. Vitunguu vikiwekwa gizani huchipua kwa urahisi.

 

2. Muozo laini

Ugonjwa huu hushambulia vitunguu baada ya kukomaa; husababishwa na vimelea (bacteria). Vitunguu hutoa harufu mbaya ya uozo.  Kuepuka hilo vuna kwa wakati unaofaa, hifadhi sehemu yenye mwanga na hewa inayozunguka.

 

Mavuno

Mavuno ya kitunguu hufanyika siku 90 hadi 150 kutegemea mbegu uliyopanda.kitunguu kinakuwa tayari kipindi majani yamedondoka na asilimia 70 ya upande wajuu umekauka na kudondoka


PIA KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU KILIMO HICHI mfano mbegu bora,uwekaji wa mbolea,udhibiti wa magonjwa,ratiba na umwagiliaji mzuri na n.k

KWA WALE WANAOHITAJI MAFUNDISHO HAYA KWA AJILI YA KILIMO HIKI WANITAFUTE KWA NAMBA HIZO CHINI.


Kwa mawasiliano zaidi

PIGA  0769550328

Whatsapp 0769550328


Barua pepe  

cheteagrosolution@gmail.com

  KARIBU SANA


Comments

Popular posts from this blog

Kilimo Bora Cha Matikiti Maji

KILIMO CHA MATIKITI MAJI toleo la pili

JIFUNZE KUHUSU KILIMO CHA KISASA CHA MATUNDA