Posts

Showing posts from November, 2020

upimaji wa udongo

Image
KUPIMA UDONGO  upimaji wa udongo ni nini? UPIMAJI WA UDONGO ni kitendo cha kujua kiasi gani virutubisho vinapatikana katika udongo bila kusahau kujua uchachu wa udongo(pH). FAIDA ZA KUPIMA UDONGO 1.Kujua kiasi gani cha mbolea kinahitajika inamsaidia mkulima kujua anahitaji kiasi gani cha mbolea katika eneo husika..Mkulima hana haja yakuanza kukisia kukisia idadi ya mbolea.mfano unaweza kukadiria kuwa mifuko katika shamba lako inatosha mitatu kumbe unatosha mfuko mmoja. 2.Kutunza rotuba ya udongo kiasi kikubwa kuwekwa katika udongo upelekea afya ya udongo kudhorota na kupelekea rotuba kupungua...Mfano matumizi makubwa ya  UREA katika shamba inaweza kupelekea uchachu wa udongo kuwa mkubwa na hivyo kusababisha rotuba kupungua. 3.Kuongeza uzalishaji katika shamba lako kila zao linahitaji kiasi stahili cha virutubisho,ko endapo ukaweka mbolea kwa makadirio inaweza kusababisha zao husika kupata kiwango cha chini cha kirutubisho na kusababisha mavuno kuwa machache.Na pia unaweza kuweka kiwang

KILIMO CHA NDIZI

Image
UTANGULIZI KILIMO CHA NDIZI ili uweze kulima kibishara licha ya kuwa na changamoto za magonjwa na wadudu basi kinahitaji ufuate mbino Bora za kilimo. Mbinu Bora za kilimo kinaendana na uchaguaji wa mbegu bora ambazo hazina vimelea vya magonjwa mbalimbali pia zenye kuimili mihangaiko yoyote itakayo tokea Kama mvua nyingi au mvua chache,baridi au joto kali na pia upepo... Pia tunalenga katika uzalishaji wa kiasi kikubwa ambacho ndo kiini cha lengo la kupanda migomba ,migomba inayo itajika ni ile ambayo huzaaa kwa kiasi kikubwa ili uweze kupata kipato kikubwa. VITU MUHIMU Ndizi(vidole) hukaa katika makundi madogo inayoitwa kichana huwa na ndizi(vidole) 20 ambayo mkungu mmoja huchukua vichana kuanzia 3 hadi 20 kwa wastani..kutokana na Aina tofauti tofauti za migomba uzito wa mkungu  kuanzia  kilo 30 Hadi 50. Tunaaina mbili za migomba 1.migomba ya kienyeji 2.migomba ya kisasa 1.Migomba ya kienyeji Hiii hotolewa kutoka kwa mama..mfano mzuzu,mshare,kisukari,mkono wa tembo n.k 2.migomba  ya ki